Jul 10, 2013

WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO- 2013

 
 Muhula wa kwanza kwa wanafunzi wa Kidato cha Tano kuanzia mwaka huu 2013 itaanza mwezi Julai. 


Wanafunzi wamepangwa katika shule zenye miundombinu na walimu kwa masomo husika. 


Aidha, kama baadae upungufu utajitokeza, wakuu wa shule wameelekezwa kufanya taratibu za kuazima walimu wa muda na kutoa taarifa kwa uongozi wa halmashauri husika kuhusu upungufu wa walimu uliopo. 


Kwa nafasi hii, ninaagiza wanafunzi wote kuripoti katika shule walizopangwa tarehe 29 Julai, 2013. Kama kutakuwa na sababu yoyote ya msingi ya kuhamia shule nyingine, uhamisho wa kawaida utafanywa baada ya kuripoti shuleni kupitia kwa mkuu wa shule husika, Mkurugenzi wa Halmashuri/Manispaa na Katibu Tawala wa Mkoa.

 (Wizara haitabadilisha shule walizopangwa wanafunzi)

Wanaporipoti wanatakiwa kuwa na:
   Original Result slip na Living Cerificate


PHILIPO A. MULUGO (MB)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
10 Julai, 2013



WASICHANA....<<<  BOFYA  HAPA>>


WAVULANA....<< BOFYA  HAPA>>> 

 >>Ukitaka  kuya  download  bofya  hapo chini

WASICHANA:  << DOWNLOAD>>

WAVULANA:  << DOWNLOAD>>

No comments: